banner image

Unabii Sehemu Ya Pili.

Ninakukaribisha sana rafiki mpendwa wa masomo ya unabii na mfuatiliaji wa hii application ya mjue sana Mungu kwa hakika ukiwa tayari utamjua kwelikweli ,Tunaanza Kitabu cha Danieli kama nilivyokudokezea hapo awali hiki kitabu kinahusu nyakati zetu  hizi za mwisho.  Hivyo Kuelewa mambo yaliyo mbele yetu ni muhimu sana,kama wasafiri yatupasa kujua mwanga wetu na namna hasa mambo yanavyoendelea kwa njia hii tutapata kujua ama tutapata uzima  wa  milele,  ama  mauti  ya  milele katika mkabala wetu na matukio hayo yanayokuja.  Hivyo si suala dogo kujifunza unabii wa  kitabu  cha  Danieli  kwa  wote  wanaotaka  uzima  wa  milele.    Tukijikumbusha wakati Yesu  akizungumza  na wanafunzi  wake  juu  ya  matukio  ya  siku  za  mwisho  alisema,   "Basi  hapo  mtakapoliona Chukizo  la  Uharibifu, lile  lililonenwa  na Danieli,  limesimama mahali  patakatifu  (asomaye na  afahamu)".   Mathayo 24:15.  Ninakuomba tuanze kwanza na hii hatua uangalie Kwa makini hasa maana ya maneno haya " chukizo la uharibifu" Pia kumbuka kwamba katika haya yote kuna  hatari  kubwa mbele  yetu!  Yesu  anataka kila  asomaye alifahamu  Chukizo  hilo  la  Uharibifu  linalokuja ili atakapoliona akimbie kuokoa  maisha  yake (Mt. 24:16-22).   Chukizo la  Uharibifu  limetajwa  mahali  patatu  katika  kitabu  cha  Danieli (Dan. 9:26,27;  11:31;  12:11).  Mpendwa msomaji hili chukizo la uharibifu  Lina  majina  mengi  katika  kitabu  cha  Danieli  na  cha Ufunuo-----    Pembe  Ndogo,   Mnyama, na  kadhalika.   Utashangaa kujua  kwamba  "mnyama" katika lugha ya taaluma ya unabii sio  tusi wala kashfa kama wengi  wanavyodhani.  Maana yake ni "mfalme au ufalme" (Dan.7:17)kama tutakavyoona Kwa upana katika sura hii tukiifikia.  Biblia inajitafsiri yenyewe! Hivi maana ya

"chukizo" ni nini?  

Soma 2  Wafalme  21:1-11  na  Kumbukumbu  la Torati 18:9-14.    Kumbe!   Chukizo  ni kuabudu  sanamu,  kuwaomba  wafu,  kushughulika  na mapepo, uchawi  au ushirikina,  kuabudu jua na  nyota za mbinguni,  na kadhalika.   Mataifa, yaani, wapagani  hufanya  mambo hayo.  

Je!  "uharibifu"  ni  nini?

 Sio  kuharibu vitu,  bali ni kuwaangamiza, yaani, kuwaua  watu  (Dan.8:24,25).    
Kwa  hiyo,  Chukizo  la  Uharibifu  ni mamlaka au  utawala  au ufalme  unaoabudu  sanamu, unaowaomba  wafu,  ulio  na ushirikina, na, zaidi ya  hayo, unaowaangamiza  "watakatifu",

Lakini pia tuangalie watakatifu ni watu gani ,  "hao wazishikao  Amri  [Kumi] za Mungu na Imani ya Yesu (Ufu.14:12;  Kut. 20:3-17;  Yak. 2:10-12).
Pia nyakati za Paulo aliliona hili chukizo ndio maana analiita   "mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu [mwuaji], mpingamizi [au Mpinga Kristo]
 (2 The. 2:3,4].
Bila shaka umeanza kupata picha hasa juu ya haya maneno,  kila  mtu atapata  kumjua  huyo mpinga Kristo, kabla  Yesu  Kristo  hajarudi (tutajifunza zaidi hapo mbele) hapa  duniani.    Tutaendelea kusumbuka  na  magonjwa,  umaskini,  na  dhiki mpaka atakapokuja mwokozi wetu baada ya huyo mwana wa kuasi kutokea.
Je!    si  jambo  la  muhimu  kabisa  kuijua mamlaka hiyo ili kujua la kufanya kuokoa maisha yetu, si yale ya kimwili, bali  ya  kiroho ili tupate  kuishi  milele?  (Mt. 10:26-33;  Yoh.6:39-40;  Ufu.12:11).   Kufa  au kutokufa  si  hoja, bali kujiweka tayari kumlaki  Yesu Kristo atakapokuja  juu ya mawingu  ya mbinguni (Ufu. 2:10;  Mt. 24:29-31).

Mpendwa Msomaji, je!  kwa neema  yake  Mungu  unataka  kuwa tayari kujiunga na watakatifu  ulimwenguni kote?   Hao wazishikao amri na imani ya yesu ,Somo la Amri litatolewa ndani ya masomo haya utaelewa vizuri, je, unataka kujifunza zaidi unabii wa biblia ,usipate shaka Karibu na endelea kufuatilia ukurasa huu wa masomo ya unabii ,kumbuka  Kabla  hujaanza  kusoma  somo, omba  ili  Mungu  akupe  Roho  wake  atakayekufundisha  kweli  yote  (Yohana  16:13-15). Mungu na akubariki! Mpendwa msomaji na mfuatiliaji wa unabii huu .

Karibu Kwa kuanza sura ya kwanza ya Kitabu cha Daniel.
Unabii Sehemu Ya Pili. Unabii Sehemu Ya Pili. Reviewed by Unknown on April 10, 2018 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.